https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, June 17, 2013

Kutana na Binslum, mdau wa soka aliyepania kuinyanyua Coastal Union ya Wagosi wa Kaya

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
ILI timu iweze kufanya vizuri, kunahitaji vitu vingi, kama vile uongozi bora, sambamba uwezo wa kuingiza chochote kitu, maana mpira wa siku hizi ni fedha.
Nassor Ahmed BinSlum
Bila kuwa na fedha, ni ngumu timu yoyote kufanya vizuri, ndio maana hata Azam FC, imeweza kufanya vizuri na kutishia uwepo wa timu vigogo kwasababu inajimudu kiuchumi.
Timu ya vijana ya Coastal Union, ikijifua uwanjani.
Zipo timu ambazo zinashindwa kutikisa, maana zinakabiriwa na njaa katika mifuko yao, kama vile Villa Squad, Ashanti FC, Toto African na nyinginezo zinazowania nafasi ya kucheza ligi kuu, ukiacha zile zinazomilikwia na 
Kampuni au taasisi, kama vile Kagera Sugar, Mtibwa Sugar, JKT Orjolo, Ruvu JKT, Mgambo Shooting na nyinginezo.

Hali hii kwa sasa haipo tena ndani ya Coastal Union, yenye maskani yake jijini Tanga, maana ina mdau, Nassor Ahmed ‘Bin Slum’, ambaye kwa kupitia moyo wake, mapenzi yake dhidi ya Wagosi wa Kaya hao, mambo yanaonekana mazuri.

Tangu mwaka 2008 alipoongeza mapenzi na msaada kwenye timu hiyo, haijashuka tena daraja, sanjari na kusajili au kutumia kila wanachohitaji, ikiwa ni pamoja na kumudu kuwalipa mishahara wachezaji wote wanaokipiga Coastal Union.

Akizungumza mwishoni mwa wiki iliyopita, Bin Slum ambaye ni Mkurugenzi wa Ufundi pamoja na Mdhamini wa Coastal Union, mdau huyo na mnazi mkubwa wa timu hiyo anasema alianza zamani kuisaidia timu hiyo kutokana na mapenzi makubwa aliyokuwa nayo.

Anasema kuwa hapo awali alitaka kukipiga Coastal Union, lakini baada ya kupata ajali yaa kuumia goti uwanjani, ndoto yake ilitoweka rasmi na kubaki kama shabiki mkubwa wa mpira wa miguu, hususan kwenye timu hiyo ya nyumbani kwao.

“Coastal Union ni timu yangu ya nyumbani, nimezaliwa na kusomea Tanga, hivyo nadhani bado nahitaji kufanya kila niwezalo katika kuhakikisha kuwa inasonga mbele.

“Hapo zamani nilikuwa nafanya siri, lakini ukimya huo uliondoka na kuona nijitangaze tu kuwa msaada unatoka ndani ya Kampuni yangu ya Binslum Tyres Company Ltd, ingawa nakiri kuwa siisaidii Coastal nikiangalia faida kwa muda huu, maana ni wazi haiwezi kupatikana,” alisema BinSlum.

Mdau huyo anasema msimu wa 2011 na 2012 waliweza kufanya vizuri na kushika nafasi ya tano katika msimamo wa ligi licha ya malengo yao kulilia wasishuke daraja, ila msimu wa 2012/2013 hali imebadilika baada ya kuambulia naafsi ya sita.

Anasema si matokeo mabaya kwa timu yao, maana timu kama Coastal Union ina changamoto nyingi, ikiwamo uwezo wa kifedha, malengo na ushirikiano kwa wachezaji wake.

BinSlum anasema kuwa tayari wameanza kufanya usajili wenye dhamira ya kuifanya Coastal inyakuwe ubingwa msimu ujao, wakimsajili Haruna Moshi Boban na Juma Nyosso wote kutoka Simba.

Wengine waliosajiliwa Coastal Union ni pamoja na Markus Ndehele na Said Lubao wote kutoka JKT Orjolo, wakati Abdallah Athuman Ally huyu anatokea Jamhuri ya mjini Pemba, ambaye pia ni mchezaji bora katika soka la Zanzibar na Kennet Masumbuko aliyesajiliwa kutoka Polisi Morogoro.

Msimamo wa Coastal Union ni kuwa hawana udugu kabisa na timu za Simba na Yanga, kama baadhi yao wanavyofikiri, isipokuwa uswahiba huo utakuwapo katika masuala ya Kitaifa.

Anasema wapo baadhi ya watu wanasema kuwa timu ya Coastal Union ina urafiki na Simba, jambo ambalo halina ukweli wowote, hivyo .
Said Lubao, wua wakati soka u wa Benchi la
 

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...