https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, June 17, 2013

DC Kipozi wa wilaya ya Bagamoyo ataka watoto walindwe


Na Mwandishi Wetu, Bagamoyo
MKUU wa Wilaya ya  Bagamoyo, mkoani Pwani, Ahmed Kipozi ameitaka jamii kuakikisha inashughulikia suala la kuwalinda watoto ikiwemo suala la ukatili, mila kandamizi na utumikishaji usiofaa.
Mkuu wa Wilaya Bagamoyo, Ahmed Kipozi, akizungumza jambo juu ya haki za watoto wilayani humo leo.

Watoto wakicheza mchezo wa kufukuza kuku.
Kipozi alisema hayo jana jumapili alipokuwa mgeni rasmi wakati wa maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika inayofanyika kila mwaka Juni 16.
Akihutubia wananchi, pamoja na watoto wakiwemo  kutoka shule mbalimbali za msingi za Wilaya hiyo, alisema kuwa Jamii inajukumu kubwa ya kuakikisha sula la ulinzi linatekelezwa kwa pamoja hasa katika kumlinda mtoto.

“Kumlinda mtoto na mila kandamizi ni jukumu letu, nasi hatuna budi kuwaakikishia hilo pamoja na kutokeza vitendo viovu dhidi yao” alisema Kipozi.

Pia alieleza kuwa wajibu wa kila mmoja ni kuakikisha watoto wanakuwa kwenye ustawi bora katika makuzi yao ilikuweza kutimiza malengo yao mbalimbali pindi watakapofika ukubwani.

kwa upande wake, mmoja wa wazee wa Mila wilayani hapa, Rashid Yusufu  Sekamba alisema kuwa watahakikisha wanaachana na mila potofu ilikuendana na wakati ikiwemo suala la unyago kwa watoto wa kike.
“Tumesikia sana kilio chenu watoto, juu ya mila potofu hasa unyago, tutachukua hatua na hata kulimaliza.

.Mimi sijui huko kwenye unyago wanafundisha mambo gani, ila kama unamcheza mtoto bado yupo shule, ni lazima aende akajaribu kwa vitendo hili si sawa. Sasa unadhani hili ni sawa?, si sawa wazee wa mila tutaangalia namna ya kuachana nalo,” alisema Sekamba.

Katika maadhimisho hayo, ambayo yaliratibiwa na Halimashahuri ya Bagamoyo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, Mkuu wa Wilaya alikabidhi baiskeli moja ya walemavu (wheelchair), pamoja na kupokea kandambili pea 300, vyote vilivyoolewa na Asasi ya TRACED.

Sherehe za mwaka huu za mtoto wa afrika yenye kauli mbiu, “Kuondoa mila potofu zenye kuleta madhara kwa watoto: Ni jukumu letu sote”.
Kwa upande wao wajumbe mbalimbali waliotoka asasi za kiraia ndani ya wilaya hiyo walipongeza shughuli hiyo.

Asasi hizo ni pamoja na HELP Foundation, Mkombozi, TRACED, HakiMtoto Foundation, BAKA, Compassion na wengine wengi.
Kwa upande wa watoto hao waliweza kuelezea na kutoa kero mbalimbali dhidi ya vitendo wanavyofanyiwa na jamii ikiwemo unyanyasaji na ukatili huku wakiomba kutambua watoto ni taifa la leo  hivyo linahitaji kulindwa.

Kupitia risala yao, watoto hao mbele ya DC, walitaka kuthaminiwa na kuwekewa ulinzi, kusikilizwa na yale yote yanayohusu haki ya mtoto.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...