https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, January 31, 2014

Maoni na mtazamo wa mwananchi wa kawaida wilayani Handeni, mkoani Tanga

Yameandikwa na Rashid Hassan Kilo, kutoka kijiji  cha Misima, wilayani Handeni, mkoani Tanga katika mtandao wa facebook.

HAYA ni malalamiko ya watu wa kijiji cha Misima, wilayani Handeni mkoani Tanga, yameandikwa na Rashid Hassan Kilo, nikaona niyapachike hapa kutoka kwenye wall yake...... Sijaongeza wala kupunguza...

Habari za asubuhi "Wana wa Handeni"

Kwangu kumekucha salama hofu na mashaka ni kwenu. Hoja yangu leo ni juu ya matangazo yaliyozagaa kila kona ndani ya mipaka ya kijiji cha Misima yanayohusu kuchangia ujenzi wa maabala ya shule ya sekondari Misima katika mchanganuo ufuatao:
1. Nguvu kazi 10,000@
2. Ng'ombe 3000@
3. Mbuzi/kondoo 1000@
Labda niishie hapo kwanza kwakuwa mlolongo ni mrefu sana kwani ni zaidi ya vipau mbele 26 na viwango tofauti vya kulipia. Mwisho ni jina Mtendaji wa kijiji
S. KIDUNDA
VEO-MISIMA.
Japo tunajuwa haya ni maendeleo lakini kwanini tusingeitishwa mkutano na kupata ufafanuzi juu ya ghalama za ujenzi wa maabala hiyo, gawanya kwa idadi ya watu, mifugo, maduka, migahawa na vyanzo vyote vya vijiji 5 vya kata ya Misima?

Katika ibara ya 18(d) ya Katiba tuanayotumia sasa ya 1977 "Kila mtu anayo haki ya kupewa taarifa wakati wowote kuhusu matukio mbalimbali muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na pia kuhusu masuala muhimu kwa jamii."

Leo hili lakujenga maabala ni tukio muhimu sana kwetu na kwa vizazi vyetu ila jinsi ya uongozi wa kiimla wa Misima unavyotufanyia umeyatokomeza na unazidi kuyatokomeza kabisa maendeleo ya Misima.

Leo hii ni miaka mingi imepita bila kusomewa mapato na matumizi, lakini pia ni zaidi ya mwaka 1.6 tangu 18/10/2012 hatujafanya mkutano kwa viongozi kutuogopa kwa maovu yao, leo hatupo tayari kuchangia bila kupata mchanganuo unaoeleweka lakini pia hatupo tayari kutoa pesa kwa kwa viongozi wasio waaminifu.

Lakini la mwisho kiwango kilichowekwa ni kikubwa bora ingekuwa kila kaya 10000, lakini nguvu kazi? Kwa kipindi hiki ambacho wachangiaji wenyewe wanategemea chakula cha msaada toka serikalini? Ningeomba viongozi wangefanya mkutano kwanza na wanakijiji ili kujadiliana kwanza kuliko kutuogopa, mtatuogopa hadi lini?

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...