https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, January 26, 2014

Madabida mgeni rasmi Diwani Cup



Na Kambi Mbwana, Dares Salaam
MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida leo atakuwa mgeni rasmi katika mashindano ya Diwani Cup yatakayofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Mbagala Kuu, iliyopo katika Kata ya Mbagala Kuu.
Timu za Kuzazi na Sansiro kutoka kata hiyo zitapambana kuwania zawadi ya kombe, ng'ombe na jezi seti ambazo ni zawadi za mshindi wa kwnza.

Madabida ndiye atakayekabidhi zawadi ya mshindi wa kwanza na ile ya pili ambaye ataondoka na jezi seti moja huku msindi wa tatu atapewa jezi seti moja.

Akizungumza jana, Diwani wa Kata ya Mbagala Kuu, Benson Malawandu, ambaye ndiye mwandaaji wa mashindano hayo alisema fainali hiyo inatarajiwa kuwa ya aina yake kutokana na kukutanisha timu zenye upinzani wa jadi.

Alisema kilichopelekea kumwalika Madabida katika mashindano ni kutokana na kiongozi kuwa ni mpenda michezo ambaye amekuwa akitoa kuhakikisha anasaidia vijana.
Malawandu akizungumzia mashindano hayo kwa ujumla alisema kwa kiasi kikubwa malengo yametimia.

Alisema wakati anayaanzisha alikuwa na malengo ya kukutanisha vijana pamoja, kutoa fursa kwa vijana kutumia michezo kwa ajili ya kujenga mshikamano na kuepukana na kukaa kwenye magenge.

"Malengo ya mashindano haya kwa asilimia kubwa yamefanikiwa sana, na ndio maana hata zawadi za washindi zilianza kutoka katika hatua za makundi kila timu iliiyoongoza ilipata jezi seti moja na mpira na zile za pili zilipata mipira," alisema.

"Pia kila timu iliyoshiriki nilitoa mpira mmoja kwa ajili yao kujiandaa, na katika hatua ya robo fainali kila timu pia ilipata zawadi ili kuongeza morali ya mashindano, aliongeza.

Pia alisema lengo lingine lilikuwa ni kukamilisha ilani ya chama chao ambacho kinaichukulia michezo kama ni ajira tosha kwa vijana ambayo inaweza kuwakomboa kiuchumi.

Wakati huo huo Malawandu alisema mashindano hao kuanzia sasa yatakuwa ni endelevu na ana mpango wa kuyafanya kila mwaka huku pia kwa sasa akijipanga na kamati yake kwa ajili ya kuanzisha na wanawake.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...