https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, January 19, 2014

Wadau wa masumbwi wapewa somo


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

MAPROMOTA wa mchezo wa masumbwi wameombwa kuwa makini na waaminifu ili wahakikishe wanasimamia vyema na kuendeleza sekta hiyo ili kuuletea mafanikio ndani na nje ya nchi.


Hayo yamesemwa na mdau wa ngumi ambaye pia ni jaji wa masumbwi, Ibrahim Kamwe, alipozungumza na gazeti la Mtanzania Jumapili, ikiwa ni miezi kadhaa baada ya kudaiwa kuwa muandaaji wa pambano la Francis Cheka na Phil Williams, ambaye ni Jay Msangi, kulivuruga.


Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Kamwe alisema kuwa ni wakati wa mapromota kujitahidi katika maandalizi ya mapambano yao, sanjari na kuwalipa mabondia na wote wanaostahili ili kuepusha lawama.


“Katika pambano la Cheka na Williams kulikuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wadau, akiwamo Williams mwenyewe, hivyo huu ni wakati wa kuliangalia jambo hilo kwa ajili ya kulinda heshima ya mchezo wa ngumi.


“Tusipokuwa makini hata wale wachache wanaojituma katika masumbwi watashindwa kuwekeza zaidi kutokana na imani kuwa mchezo huu unaendeshwa bila kuzingatia vigezo na mahitaji ya mafanikio yake,” alisema.


Kwa mujibu wa Kamwe, katika pambano la Cheka na Williams lililolalamikiwa, yeye alikuwa msimamizi mkuu.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...