https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, January 28, 2014

Wadau wa ngumi wasifia mkutano wao


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

KATIBU wa Ngumi za Kulipwa hapa nchini, Ibrahim Kamwe, amesema kwamba mkutano wao utakaofanyika Februari Mosi mwaka Vijana Hall Kinondoni, utakuwa na faida kubwa ya kujadili sekta hiyo ya masumbwi.


Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Kamwe alisema kwamba mkutano huo umepewa Baraka zote na Rais wa Oganaizesheni ya ngumi za kulipwa (TPBO), Yasin Abdallah.


Alisema kuwa anaamini wadau wote wa masumbwi, wakiwamo mapromota watajumuika pamoja kutafuta namna bora ya kuendeleza mchezo wa masumbwi hapa nchini.


“Huu ni mkutano wa kwanza unaofanyika nchini huku ukiwa na manufaa makubwa kwa sisi wadau wa masumbwi hapa nchini, hivyo naomba tujiandaye vizuri kwa maendeleo yetu.


"Mkutano utaanza mapema asubuhi, huku nikiamini kuwa kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa, ukizingatia kuwa mbali na mapromota, pia mabondia na makocha wa ngumi ni miongoni mwa wanaotarajiwa khudhuria,” alisema Kamwe.


Mchezo wa masumbwi unatajwa kati ya ile iliyopunguza makali yake, licha ya wadau mbalimbali katika tasnia hiyo kuendelea kuupigania ili ubaki katika mafanikio yake kama zamani.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...