https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, January 15, 2014

Coastal Union waanza mazoezi ya gym Uwanja wa Sultan Qaboos, Muscat Oman



Na Mwandishi Wetu, Oman
KLABU ya Coastal Union jana ilianza programu ya Gym katika uwanja wa soka wa Sultan Qaboos, jijini Muscat. Coastal Union ambayo ipo Oman kwa kambi ya wiki mbili kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi kuu Tanzania bara, imeamua kufanya mazoezi ya gym kuhakikisha wachezaji wake wanakuwa na misuli imara ili kukabiliana na mikiki ya mechi. 


Hafidh Kido, ambaye pia ni msemaji wa Costal Union.
Akizungumza na Handeni Kwetu Blog, kocha wa Coastal Union, Yusuf Chipo amesema anajua watu wakisikia hivyo wataogopa na kuanza kuwakamia lakini hana budi lazima afanye hivyo.
"Wewe unanisababishia balaa Tanzania, yaani najua timu nyingine zikisikia na kuona hivi watakamia, lakini hii ndiyo hali halisi vijana lazima wapige chuma wawe imara.

 "Unajua tumefanya mazoezi mengi uwanani, gym inasaidia kulainisha na kuifanya misuli kuwa imara. Hii ndiyo njia pekee ya kuwasaidia," alisema Chipo.
Nae daktari wa timu Dk. Francis Mganga, amemwambia mwandishi wetu kuwa anafurahi kuona kile kitu alichohitaji kwa kipindi kirefu sasa kimetimia. 

"Hiki niliwashauri viongozi kwa muda mrefu, wachezaji hawana nguvu, kunyanyua vitu vizito kunaimarisha misuli. Naamini sasa mambo mazuri, kwasababu hata mchezaji akianguka hawezi kuumia kizembe ikiwa misuli yake ni imara," alisema. 

Katika upande mwingine meneja wa Coastal Union, Akida Machai aliliambia Raia Tanzania kuwa, atahakikisha ananunua vifaa vya Gym ili timu iwe na gym yake.
"Gym ni muhimu, hata mimi nimeona, tutaangalia mfuko wetu umekaaje ili tukirudi tutengeneze gym yetu wenyewe. pale klabu tuna eneo kubwa tunaweza kununua vifaa na kuanzisha. hata kule kambini pia tuna vyumba vikubwa," alisema.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...