https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, January 08, 2014

Mapacha Watatu waukumbuka 2013 kwa matukio manne


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

BENDI ya Mapacha Watatu, inajivunia kumaliza mwaka 2013 kwa kufanya matukio manne makubwa na kudhihirisha ubora wao katika tasnia ya muziki wa dansi hapa nchini.

Vijana wa Mapacha Watatu pichani.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Meneja wa bendi hiyo, Khamis Dacota, alisema kwamba matukio hayo yaliandaliwa kwa ubora bila kuangalia changaamoto zozote wanazokutana nazo.

Alisema mwaka huo wa 2013 uliomalizika waliweza kuzindua albamu yao ya Yarabi Nafsi, Cindy VIP Show, Kumbukumbu ya kuzaliwa Mapacha Watatu pamoja na tukio la kumkaribisha mwimbaji wao Catherine Cindy kutoka ughaibuni.

“Haya ni mafanikio makubwa ambayo tuliweza kuyaandaa kwa kiwango cha juu na kudhihirisha ubora wetu katika tasnia ya muziki wa dansi hapa nchini, licha ya kukabiliwa na changamoto kadhaa.

“Naamini mwaka huu utakuwa mzuri zaidi kwa upande wa Mapacha Watatu, sanjari na kuendeleza makali yetu kwa kushirikiana na wadau wote wanaotuunga mkono,” alisema.

Kwa mujibu wa Dacota, wanamuziki wake wamejipanga imara kuendeleza burudani kwa mashabiki wao kwa ajili ya kuwa kileleni kwa kushindana na bendi mbalimbali zinazofanya vizuri hapa nchini.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...