https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, January 09, 2014

Jahazi Modern Taaarab wafafanua dhumuni la kutambulisha nyimbo mpya Morogoro



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
KUNDI la Jahazi Modern Taarab limefafanua ni kwanini limeamua kuuchagua mji wa Morogoro kama kituo chao cha kwanza cha kutambulishia nyimbo zao mpya zitakazounda albam yao mpya ijayo.

Mauaji akizungumza na mwanadada Hawa Hassan kulia kwake.
Jahazi wanatagemewa kufanya onyesho maalum Morogoro kwaajili ya kuwaonyesha nyimbo mpya mashabiki wao Ijumaa ya tarehe 31 mwezi huu ndani ya ukumbi wa Tanzanite Complex.

Jana kiongozi wa Jahazi Modern Taraab Mohamed Mauji alifanya mahojiano na kipindi cha Sham Sham za Pwani cha ITV kinachoongozwa na mtangazaji Hawa Hassan (Kama wanavyoonekana pichani) ambapo msanii huyo alitoa sababu kadhaa ni kwanini wameichagua Morogoro. Kipindi hicho kitaruka hewani Jumamosi hii saa 11 jioni.

Mauji ambaye ni mcharazaji gitaa la solo miongoni mwa sababu nyingi alizozitoa ni pamoja na kusema kuwa mji wa Morogoro ni ngome yao kubwa (ukiondoa Dar es Salaam) na hivyo safari hii wameupa heshima ya kipekee.

Mara zote Jahazi imekuwa ikianza kutambulisha nyimbo mpya jijini Dar es Salaam na baadae kufuatiwa na uzinduzi na baada ya hapo ndio wanazipeleka nyimbo mpya mikoani.
Mauji pia katika mahojiano yake hayo alifichua mikakati yao mikubwa ya kukukabiliana na ushindani kwa mwaka huu wa 2014.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...