https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, January 30, 2014

Mzee Yusuph: Tumejipanga kuwapa raha Morogoro

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MKURUGENZI wa kundi la Jahazi Modern Taarab, Mzee Yusuph, amewataka wadau wa muziki wajipange imara kwa ajili ya kupokea burudani zao katika onyesho la aina yake litakalofanyika Januari 31 katika Ukumbi wa Tanzanite Complex, uliopo mjini Morogoro.
Mzee Yusuph, pichani.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mzee Yusuph, alisema kuwa amejipanga yeye na waimbaji wake kujibu maswali kwanini wao ni vinara katika muziki huo.

Alisema kuwa mkoa Morogoro ni kati ya ile inayopenda muziki wao, hivyo suala hilo limemfanya aone shauku ya kufanya kazi nzuri jukwaani kwenye onyesho hilo.

“Nimejipanga imara kama Mkurugenzi  kuwapatia burudani kabambe wadau na mashabiki wetu katika onyesho la mkoani Morogoro ambapo tutafanya vitu vya aina yake.

“Tutaimba nyimbo zetu mpya na zile za zamani ambapo wadau wetu wana kila sababu ya kuja kupata vitu vya aina yake kutoka kwetu Jahazi, lenye waimbaji hodari,” alisema.

Jahazi ni miongoni mwa makundi ya muziki wa taarabu yenye waimbaji wenye uwezo wa juu katika tasnia ya muziki wa taarabu hapa nchini, huku mashabiki wengi wakiwaunga mkono.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...