https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, January 30, 2014

Wadau kibao wamzika MCD mkoani Kilimanjaro



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
HATIMAYE mwili wa mwanamuziki wa zamani wa bendi ya The African Stars, Twanga Pepeta, Soud Mohamed ‘MCD’ ulizikwa jana katika makaburi ya Njolo, mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro na kuhudhuriwa na watu mbalimbali.


Wananchi na wadau wa muziki wakimzika Mpiga tumba wa zamani wa Twanga Pepeta, marehemu MCD.

Marehemu MCD alifariki juzi mjini Moshi baada ya kuugua kwa muda mrefu, huku akiacha pengo la majonzi makubwa katika tasnia ya muziki wa dansi nchini.

Akizungumza mara baada ya maziko ya MDC, Meneja wa bendi ya Twanga Pepeta, Hassan Rehani, aliwashukuru wadau mbalimbali waliofanikisha mazishi ya mpiga tumba wao huyo nguli nchini.

“Wadau mbalimbali waliweza kujitokeza kwa wingi katika vikao vya kujadili msiba wa MCD na hatimaye kufika nyumbani kwa  marehemu Moshi, mkoani Kilimanjaro.

“Twanga Pepeta imepata pigo zito kwa kuondokewa na MCD, ambapo pia tunaamini kuwa uwezo wake utaenziwa na wadau wote wa muziki wa dansi,” alisema.

MCD aliwahi kufanya kazi na bendi mbalimbali, ikiwamo Mashujaa Musica, ambapo pia walishirikiana na wadau walioguswa na msiba huo mzito.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...