https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, January 21, 2014

Chaneta Tanga yatoa semina kwa walimu wa mchezo huo

Na Safari Chuwa,Tanga.
CHAMA cha Mpira wa Pete Mkoa wa Tanga,(Chaneta)kimeanza kutoa semina ya walimu wa mchezo toka wilaya zote za mkoa wa Tanga lengo likiwa ni kuwaanda walimu hao kwa ajili ya kufundisha kwenye michezo ya Umitashumta na Umiseta mkoani Tanga.

Akizungumza jijini Tanga, Katibu wa chama hicho,Julieti Mndeme alisema semina hayo ina lengo ya kuwajengea uwezo washiriki na kuhamasisha mchezo huo ambayo yanaendeshwa na mkufunzi wa toka Chama hicho Taifa Anna Kibira.


Mndeme alisema semina hiyo itaendeshwa kwa muda wa siku kumi na moja  yalianza Januari 16 na  yanatarajiwa kuhitimishwa Januari 27 mwaka huu na yanashirikisha wanawake na wanaume yakifanyika kwenye viwanja vya bandari mkoani hapa.

Katibu huyo alisema mikakati waliokuwa nayo katika kuuendelea mchezo  huo ni kuanzisha ligi za vijana wadogo na kuweka msukumu kwenye mashindano mbalimbali yakiwemo ya wilaya na mkoa ili kuupa maendeleo mchezo huo.

Mndeme alisema kuwa ni matumaini yake mpaka mashindano hayo
yatakapomalizika watapatikana walimu wazuri ambao watakuwa ni chachu ya kukuza maendeleo ya mchezo huo kwenye wilaya wanazotoka na mkoa kwa ujumla.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...