https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, January 19, 2014

Super D: CD za masumbwi zitahamasisha ngumi

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

KOCHA wa mchezo wa masumbwi nchini, Rajabu Mhamila ‘Super D’ amesema kuwa lengo la kuamua kutengeneza CD zinazochanganya mapambano ya mabondia mbalimbali ni kuongeza chachu ya vijana kujiingiza katika tasnia hiyo inayosua sua kwa sasa.


Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, alisema kuwa CD hizo za masumbwi zinaweza kuongeza hamasa ya wakubwa na wadogo kupenda kucheza ngumi kwa kuona mapambano hayo.


“Mchezo wa masumbwi kwa Tanzania umekuwa ukisua sua mno, hivyo tangu mwanzo nikaamua kuja na wazo hili ambalo kwa kiasi kikubwa linatoa fursa nzuri kwa wadau wote.


“Nawaomba wadau na mashabiki waweze kupata CD hizi katika mapambano mbalimbali yanayofanika nchini, huku CD hizo zikionyesha picha halisi ya wakali wa masumbwi ndani na nje ya nchi,” alisema Super D.


Mbali na shughuli hiyo ya kutengeneza CD, Super D ni kocha wa masumbwi anayetokea katika club ya Ashanti yenye maskani yake Ilala, jijini Dar es Salaam.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...