https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, January 23, 2014

Coastal Union kurejea nchini leo tayari kwa patashika ya ligi


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

KLABU ya Coastal Union ‘Wagosi wa Kaya’, kurejea nchini leo saa kumi alasiri kutoka Muscat, Oman kwa ndege ya shirika la Oman Air. 

Taarifa ya Mwenyekiti wa Coastal Union Hemed Hilal ‘Aurora’iliyotumwa katika vyombo vya habari inasema timu yao ikiwa nchini Oman imepata mafunzo na mapumziko mazuri kutokana na ratiba nzuri iliyopangwa na kocha wao Yusuf Chipo. 

Alisema kuwa Wagosi wa Kaya walikuwa Oman kwa wiki mbili sasa, waliwasili nchini humo Alhamisi ya Januari 9 mwaka huu, huku wakirejea leo Alhamisi ya Januari 23, kwa ajili ya kuanza mbio za Ligi ya Vodacom, ambapo mzunguuko wa pili utaanza Jumamosi.

 “Nashukuru malengo yetu yametimia, sitaki kuahidi mengi lakini naamini wapenzi wa Coastal Union, watajionea wenyewe matunda ya kambi hii ya wiki mbili. 

Wagosi, wanaoshika nafasi ya nane katika ligi kuu walicheza mechi ya awali dhidi ya Al Mussannah Club inayoshika nafasi ya saba katika ligi kuu ya hapa, Wagosi wakatoka na ushindi wa mabao 2-0. Mechi ya pili walicheza na timu iliyo daraja la kwanza iitwayo Oman Club, nao waliambulia kibano cha mabao 2-0 kutoka kwa Wagosi wa Kaya,” alisema. 

Mechi ya tatu Wagosi walikumbana na kisiki cha Fanja Club inayoshika nafasi ya tano katika ligi ya Oman, ambapo coastal Union walipokea kichapo cha bao moja kwa ubuyu. Katika mechi ya nne nay a mwisho Coastal Union, ilitoa suluhu ya bila kufungana na timu ngumu ya Oman inayoshika nafasi ya nne

Mechi ya kwanza mzunguko wa pili Wagosi watacheza na JKT Oljoro katika uwanja wa mkwakwani Januari 25 siku ya Jumamosi, na siku ya Jumatano Januari 29 Wagosi watashuka dimbani kumenyana na Yanga ya jijini katika uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...