https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, January 28, 2014

Jumuiya ya Wazazi CCM Wilayani Kongwa yajipanga


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

JUMUIYA ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilayani Kongwa mkoani Dodoma, Januari 29 itaandaa mechi ya kirafiki itakayokutanisha timu za Kata ya Segeri kwa ajili ya kusherehekea miaka 37 ya CCM tangu kuzaliwa kwake inayoadhimishwa Februari tano kila mwaka.


Akizungumza jana kwa njia ya simu kutoka mkoani Dodoma, Katibu wa Jumuiya hiyo, Hussein Mwaikambo, alisema kuwa lengo la mchezo huo ni kuwakusanya wadau wa michezo na kutafuta fursa ya kusherehekea kwa pamoja kuzaliwa kwa CCM.


Alisema kuwa lengo lao ni kutumia fursa hiyo kufurahia kuzaliwa kwa chama chao, wakiamini kuwa vijana watapata nafasi ya kubadilishana mawazo na kujiweka sawa kiafya.


“Katika kuelekea miaka 37 ya CCM ambapo kwa mwaka huu sherehe hizi zitafanyika mkoani Mbeya tumejipanga kwa sisi wilaya ya Kongwa kujipanga kwa vitu vingi ikiwapo mechi ya kirafiki ambayo wakati huu maandalizi yake yanaendelea.


Hili litakuwa tukio muhimu ambalo litatangazwa litakapokamilika, hasa kwa timu zitakazochaguliwa ambazo zitacheza baada ya vitu vyote kufanyika asubuhi hadi jioni,” alisema.


Kwa mujibu wa Mwaikambo, taratibu zote za sherehe hizo zitaendelea kuratibiwa ili kuhakikisha kuwa tukio hilo la burudani na michezo linafanyika kwa mafanikio makubwa.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...