https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, January 24, 2014

Tiketi za Elektronik zakwama Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, viwanja vingine bam bam

Viwanja vyote ambavyo tayari vimefungwa mfumo wa elektroniki vitatumia tiketi za elektroniki isipokuwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambao wenyewe utachelewa kidogo ili kuangalia kwanza mfumo huo unavyofanya kazi katika viwanja vingine.
Rais wa TFF, Jamal Malinzi, pichani.
Kwa viwanja vinavyotumia mfumo huo tiketi zinanunuliwa kupitia mtandao wa Vodacom ambapo mteja ni lazima awe amesajiliwa katika MPESA. Ataanza kwa kupiga *150*03*02# ambapo atapewa namba ya kumbukumbu anayotakiwa kuihifadhi kwani ataulizwa wakati anafanya malipo kwa kupitia MPESA ambapo ataingia kama kawaida kwa kutumia *150*00#.

Baada ya kulipa atapewa namba ya tiketi ambapo atakwenda kwenye mashine maalumu za kuchapa (printer) ambazo ziko katika vituo mbalimbali na kuchapa tiketi hiyo ambayo ndiyo atakayokwenda nayo uwanjani.

Njia nyingine ya kununua ni kwa wateja wa benki ya CRDB ambayo wamejisajili kwenye simbanking. Wao wataingia kwa kutumia *150*03# na kufanya malipo ya tiketi. Nao baada ya kupata namba watakwenda ku-print tiketi kwenye mashine hizo maalumu.

Vilevile tiketi zinapatikana kupitia maduka ya CRDB Fahari Huduma ambayo yapo katika maeneo mbalimbali nchini. Watakaonunua kupitia maduka hayo watapata tiketi na kwenda moja kwa moja uwanjani.

DAR ES SALAAM
Kwa mechi za Dar es Salaam (Uwanja wa Azam) ambao ndiyo unaanza kutumia tiketi za elektroniki maduka ya CRDB Fahari Huduma yanayouza tiketi hizo ni; 1 Shs Distributors Limited (Mtoni Kwa Aziz Ally), ABC Computer (Mtaa wa Samora), Abdi Ally Abdi (Kariakoo), Aika- El Traders (Africana), Amaly Investment (Mtaa wa Sikukuu, Kariakoo), Athuman Fakhi Adam (Kongowe, Mbagala) na Bemuda Supplies Agency (Tegeta- Kibo Complex).

Benedict Traders (Barabara ya Uhuru/Lumumba), Ellytex Investment (Mtaa wa Indira Gandhi), Fedha Investment Limited (Pamba Road), Fuya Godwin Kimbita (Tegeta Block E), Hakika Limited (Mtaa wa Swahili, Kariakoo), Irice Stationary (Tegea Kwa Ndevu), Joshua Andrew Kisamo (Mtaa wa Kongo, Kariakoo), LB Pharmacy (Mtoni Kijichi) na Lista Phares Barnabas (Tabata Segerea).

L.M.S. Agro Chemical (Sokoni Kariakoo), Matei Laurent Kiria (Mbuyuni, Kinyerezi), Michael Elisante Mchomvu (Mtaa wa Sikukuu, Kariakoo), Palmall General Supplies (Barabara ya Shekilango), Rafabi Communications (Mtaa wa Livingstone, Kariakoo), Therry Inestment Limited (Tegeta Kibaoni) na Wemerick Independent Vehicle Diagnostic Company Limited (Mtaa wa Boko).

Mashine za kuchapia tiketi zipo matawi ya CRDB Azikiwe, Holland House (mashine mbili), Kariakoo, Tabata, Tegeta, Mbezi beach, Vijana na Quality Center. Mashine nyingine maeneo ya ATM ya Mtaa wa Shaurimoyo (mbili), Kawe Oilcom, Tabata Camel, Manzese, Ubungo Oilcom, Sabasaba na Mbagala Oilcom.


BUKOBA
Maduka ya CRDB Fahari Huduma ni Tak-Biir Investment Company (Mtaa wa Jamhuri, Bilele), Mary Mother of Peace Buhembe School (Sido Block, Rwamishenye), Muleba Secretarial Bureau (Nyerere Road), Akimu Abdallah Tirutoijwa (Mtaa wa Forodhani), Jamila Rajabu Songoro (Mtaa wa Jamhuri, Bilele), Rukia Kassim Mohamed (Mtaa wa Kashai, Kashenye) na Novath Michael Kibira (Uganda Road, Majengo).

Mashine tatu za kuchapia tiketi (printers) zipo Benki ya CRDB Tawi la Bukoba.

TANGA
Maduka ya CRDB Fahari Huduma ni Fax Auction Mart (Sabasaba Ground, Korogwe Road) na Rozalia Aloyce Masanja (Usagara, Block K). Mashine tatu za kuchapia tiketi (printers) zipo Benki ya CRDB Tawi la Tanga.

MBEYA
Maduka ya CRDB Fahari Huduma ni Blue Bird Bureau de Change (Lupa way), Meenda Pharmacy Limited (Maendeleo), Access Computer Limited (Lupa way, Sisimba) na Japhes James Mwanjisi (Mtaa wa Njisi). Mashine za kuchapia tiketi (printers) zipo Benki ya CRDB Tawi la Mbeya (mbili), Tawi la Mwanjelwa na Uyole.

MOROGORO
Duka la CRDB Fahari Huduma ni Shambani Graduates Enterprises Limited (Kihonda) na pia kutakuwa na gari za CRDB (Mobile bank). Mashine za kuchapia tiketi (printers) zipo Benki ya CRDB Tawi la Morogoro, Msamvu na Morogoro Agency.

ARUSHA
Maduka ya CRDB Fahari Huduma ni Fanuel John Andrew (Arumeru, Maji ya Chai), Robert William Maeda (Arumeru, Usa River), Wakwetu General Supplies (Mtaa wa Ngongongare, Arumeru), Wallace Ndawonga Mtawa (Kimandolu Suye), Side Corner Multi Business (Levolosi, Makao Mapya Street) na Albertha Ibrahimu General (Usa River Bus Stand).

Mashine za kuchapia tiketi (printers) zipo Benki ya CRDB Tawi la Arusha (mbili), Tawi la Meru, TFA, TRA Mapato na Ngaramtoni.

MWANZA
Maduka ya CRDB Fahari Huduma ni Majura General Supplies (Mecco Street), Prisca Joachim Kitani (Gilishi Street), Niche Consult (Nyerere Road), Deogratias Just Silayo (Malimbe, Mkolani), Yohana Ndili Mahago (Igoma Mashariki), Emily Elias Sambo (Sweya Street), Y Financing Limited (Kilimahewa) na Mangare Office Solutions (Station Road).

Makoye E. Serikali (Ilemela, Kiseke Street), Elizabeth George Kiwia (Uhuru Road), Mwalimu General Services (Kitangiri Road), George Edward Mulambo (Pasiansi), Nginila Office Solutions (Rufiji Street), Elvando IT Solutions (Nkrumah, Nyamagana), Sarimosa Company Limited (Kaluta Street) na Sahara Trasport and Scrappers Dealers (Mission, Pamba Road).

Mashine za kuchapia tiketi (printers) zipo CRDB matawi ya Mwanza, Nyerere na Mwaloni wakati nyingine zipo Nyanza, Buzuruga na Ilemela.

ONYO KWA MAKOCHA, MAOFISA HABARI
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawakumbusha makocha na maofisa habari wa klabu za Ligi Kuu kujiepusha na kauli za chuki, uchochezi na uongo kwa shirikisho na waamuzi kila timu zao zinapofanya vibaya kwenye mechi.

Ni wajibu wa makocha kuzungumzia matokeo ya timu zao kiufundi badala ya kushambulia waamuzi na TFF kwa maneno makali. Pia maofisa habari nao wanatakiwa kuwa makini katika kauli zao kuhusiana na matokeo na masuala mengine.

Kwa wale watakaokwenda kinyume TFF itawafikisha kwenye vyombo vya kinidhamu na maadili kwa ajili ya kuchukuliwa hatua stahiki.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...