https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, June 06, 2013

Gwiji wa muziki wa taarabu Khadija Kopa afiwa na mume wake

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
HABARI ambazo hazijathibitishwa rasmi zinasema kuwa mume wa mwimbaji mahiri wa taarabu, akiwa ndani ya kundi zima la TOT, Khadija Kopa, Jaffari Ally amefariki Dunia, katika Hospitali ya Lugalo.

Habari ambazo hazijathibitishwa na ndugu wa marehemu, akiwamo mke wake Khadija Kopa, zinasema kuwa marehemu Ally alipelekwa Hospitalini hapo siku ya Jumatatau kwa ajili ya kupata matibabu.

Taarifa za msiba huu zinaendelea kufuatiliwa na kuandikwa kwa urefu zaidi.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...