https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, January 01, 2013

Mtanzania Leslie Liunda aula CUF







Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limemteua ofisa wake Leslie Liunda wa Tanzania, kwenda Ethiopia kukagua viwanja na hoteli ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa utaratibu wa utoaji leseni kwa klabu zitakazoziwezesha kushiriki michuano inayoandaliwa na Shirikisho hilo.

Akizungumza leo na Handeni Kwetu, Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Boniface Wambura, alisema ofisa huyo atawasili nchini Ethiopia kesho (Januari 2 mwaka huu).

Kazi hiyo anatarajiwa kukamilisha Januari 6 mwaka huu na baadaye kupeleka ripoti yake CAF.

Utekelezaji wa kazi yake hiyo nchini Ethiopia utahusisha wadau mbalimbali ikiwemo Shirikisho la Mpira wa Miguu la Ethiopia (EFF), Wizara ya Michezo ya nchi hiyo, viongozi wa klabu na mameneja wa viwanja husika.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...