https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, March 13, 2014

Yanga waitisha maandamano makubwa kulazimisha kupewa eneo la Jangwani ili wajenge uwanja wao wa kisasa, Jerry Silaa, Meya wa Ilala lawamani



BARAZA la Wazee wa Klabu ya Yanga, limetangaza kufanya maandamano makubwa siku ya Jumatatu ya Machi 17, endapo Manispaa ya Ilala itashindwa kuwajibu ombi lao la kuongezewa heka 11 katika eneo la Jangwani ili wajenge Uwanja wa kisasa wa michezo, kwa madai kuwa wanazunguushwa na wanawekewa kauzibe na serikali hiyo waliyofanikisha maendeleo yao tangu kuasisiwa kwa klabu hiyo.




Maandamano hayo yatashirikisha wanachama na wapenzi wa Yanga, kwa madai kuwa serikali imeshindwa kuwathamini na kutotambua mchango wao, licha ya klabu hiyo kujihusisha na mambo mengi ya kimaendeleo, hivyo wanaona ni fursa yao sasa kuanza kuitisha maandamano hayo makubwa.

Endapo maandamano hayo yatafanikiwa, huenda ikawa timu ya kwanza kuandamana kwa kuishinikiza serikali, huku wakitambua kuwa nchi hii inaongozwa kwa mujibu wa sheria na sio kulazimishana.
 

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...