https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, March 26, 2014

Timu ya uendeshaji wa huduma za afya wilayani Korogwe, mkoani Tanga

Meneja wa Bima ya Afya – Mkoa wa Tanga, Bw. Ally Mwakababu (kushoto) akitoa maelezo ya utangulizi wakati wa ufunguzi wa kikao cha Timu ya Uendeshaji wa Huduma za Afya ya Halmashauri (CHMT) kikijadili mchakato wa kubadirisha sheria ndogo ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kwenda katika Mfumo wa Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA). Kikao hicho cha kwanza kilifanyika jana Machi 25, 2014 katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Tanga. Pembeni ni mgeni rasmi aliyekaribishwa kufungua kikao hicho, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bw. Lewis Kalinjuna (katikati) na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya mji Korogwe, Jerry Mwakanyamale (kulia).
 Mganga Mkuu wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, Jerry Mwakanyamale (Kulia) akiongea wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bw. Lewis Kalinjuna (Katikati) katika ufunguzi wa kikao cha Timu ya Uendeshaji wa Huduma za Afya ya Halmashauri (CHMT) kikijadili mchakato wa kubadirisha sheria ndogo ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kwenda katika Mfumo wa Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA). Kikao hicho cha kwanza kilifanyika leo Machi 25, 2014 katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Tanga. Pembeni ni Meneja wa Bima ya Afya – Mkoa wa Tanga, Bw. Ally Mwakababu (kushoto).

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bw. Lewis Kalinjuna (katikati) akifungua kikao cha Timu ya Uendeshaji wa Huduma za Afya ya Halmashauri (CHMT) kikijadili mchakato wa kubadirisha sheria ndogo ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kwenda katika mfumo wa afya ya Jamii mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA). Pembeni kushoto ni Mganga Mkuu wa Halmashauri ya mji Korogwe, Jerry Mwakanyamale na Meneja wa Bima ya Afya – Mkoa wa Tanga, Bw. Ally Mwakababu (kushoto). Kikao hicho cha kwanza kilifanyika leo Machi 25, 2014 katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Tanga.
 Wajumbe wa Timu ya Uendeshaji wa Huduma za Afya ya Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Tanga (CHMT) wakifuatilia kwa makini.
 Wajumbe wa Timu ya Uendeshaji wa Huduma za Afya ya Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Tanga (CHMT) wakifuatilia kwa makini.
Wajumbe wa Timu ya Uendeshaji wa Huduma za Afya ya Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Tanga (CHMT) wakifuatilia kwa makini. 

 Mwenyekiti wa Kikao cha Timu ya Uendeshaji wa Huduma za Afya ya Halmashauri ya Korogwe, Tanga (CHMT), Bw. Salim Bori (Kushoto) akijadili jambo wakati wa kikao cha majadiliano. Pembeni ni Mwanasheria wa Halmashauri ya Mji Korogwe, Rabeca Balisidya (katikati) na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya mji Korogwe, Jerry Mwakanyamale (kulia).
Afisa Matekelezo na Uratibu wa Bima ya Afya, Singida Bw. Issaya Shekifu akiwapa uzoefu jinsi wao walivyofanikiwa kwenye mchakato wa kubadilisha sheria ndogo ya CHF kwenda kwenye TIKA na Jinsi CHF inavyofanya vizuri wilayani Iramba kwa kauli mbiu ya "Kuku mmoja CHF na matibabu mwaka mzima.
Mwanasheria wa Halmashauri ya Mji Korogwe, Rabeca Balisidya (katikati) akijadiliana jambo na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya mji Korogwe, Jerry Mwakanyamale (kulia). Picha zote kwa hisani ya Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...