https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, March 15, 2014

Ridhiwani aanza mbwembwe za kampeni Uchaguzi Mdogo Chalinzee

Meneja wa Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Steven Kazidi (kushoto) akimuinua mkono juu kwa ishara ya kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Matipwili,Saadani Wilayani Bagamoyo jana Machi 14,2014.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubi wananchi wa Kijiji cha Matipwili,Saadani Wilayani Bagamoyo,wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni zake ulioanza rasmi jana Machi 14,2014.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubi wananchi wa Kijiji cha Saadani,Wilayani Bagamoyo.wakati wa kampeni zake zilizoanza rasmi jana Machi 14,2014.

Baada ya kumaliza Mkutano na Wananchi wa Kijiji cha Matipwili,Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo Jimbo la Chalinze,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete alifika katika Kijiji cha Gongo ndani ya Tarafa ya Saadani na kukutana na wananchi wa Kijiji hicho na kuzungumza nao kama aonekanavyo pichani.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya CCM,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubia wanakijiji wakazi wa Kijiji cha Mkange,Saadani Wilayani Bagamoyo waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza huku wengi wakiahidi kumpa kura zao pindi itakapofika siku ya Uchaguzi huo mdogo wa Jimbo hilo.
Diwani wa Kata ya Talawanda ndani ya Jimbo la Chalinze,Said Zikatimu akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Gongo,huku akiwataka kutofanya ajizi pindi itakapofika siku ya Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,hivyo kura zao zote wampigie Mgombea wa CCM ambaye ni Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete.
Diwani wa Kata ya Mkange,Ndg. Abdallah Mwendali nae hakuwa nyuma katika kuwasisitiza wananchi wa Jimbo la Chalinze.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akinong'onezwa jambo na Mmoja wa kinamama wa Kijiji cha Matipwili (Jina lake halikuweza fahamika mara moja).
"Ni furaha tupu" Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akifurahia jambo na wanakijiji wa Matipwili.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akisalimiana na Wanakijiji cha Mkange,wakati alipowasili kwenye Uwanja wa Mkutano.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akisalimiana na Sheikh wa Kijiji cha Mkange.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akisalimiana na rafiki yake wa kitambo.
Mwenyekiti wa Kampeni katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ndg. Saleh Mpwimbwi akimmwagia sifa kede kede Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete .


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...