https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, March 29, 2014

Matumla alia na changamoto kwenye masumbwi


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

BONDIA wa ngumi za kulipwa hapa nchini, Mbwana Matumla, amesema kwamba mchezo wa masumbwi unahitaji uvumilivu, hasa kutokana na changamoto za ukosefu wa wadhamini.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Matumla alisema ukosefu wa wadhamini unawafanya mapromota wengi kukosa moyo wa kuendeleza mchezo huo.

Alisema kwa mabondia wanaocheza ngumi, wanapaswa kujenga ujasiri na uvumilivu mkubwa ili waweze kufikia ndoto zao katika masumbwi.

“Bila kuwa na uvumilivu mambo yanaweza kuwa magumu zaidi, maana wakati mwingine mtu anakosa pambano ili kuonyesha uwezo wake.

“Hii ni mbaya kwakuwa inashusha kiwango cha bondia husika, jambo linalotufanya sisi mabondia kupata changamoto kadhaa ya kulinda viwango vyetu,” alisema Matumla.

Matumla ni mmoja wa mabondia wenye viwango vizuri, licha ya kukutana na changamoto za ukosefu wa mapambano ya kuwania mikanda mbalimbali ndani ya nje ya nchi.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...