https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, March 27, 2014

Klabu ya ngumi yaangukia wadau wa ngumi

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

KLABU ya Ngumi ya Msisiri, yenye maskani yake Kinondoni, jijini Dar es Salaam, imeendelea kuomba hisani ya wadau wa ngumi ili kuwasaidia vifaa kwa ajili ya kumudu kuucheza mchezo huo wa masumbwi hapa nchini.


Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Kocha wa klabu hiyo, Daudi Muhunzi, alisema kwa kupata msaada zaidi wa vifaa, wanaweza kumudu kasi ya usshindani iliyopo.


Alisema klabu yao ina changamoto nyingi, hivyo wadau ni wakati wao kujitokeza kwa wingi kuwasaidia vifaa vya mchezo huo.


“Tunaomba wadau wote wajitokeze katika klabu yetu na kutusaidia kutupatia vifaa mbalimbali ili tuweze kusonga mbele.


“Naamini mpango huu ukifanikiwa, kila kitu kitakuwa kizuri kwa namna moja ama nyingine, ingawa kijana mwenzetu Yusuph Mlela, amekuwa wa kwanza kutupatia vifaa kadhaa,” alisema.


Mlela aliipatia klabu hiyo vifaa vya ngumi kama vile glove, clip bandeji, proctecta na gumshit.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...