https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, March 14, 2014

Ridhwan kuwasaidia wasanii Chalinze



Na Mwandishi Wetu, Chalinze
MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ridhwan Kikwete amesema atahakikisha anaitumia sanaa kama bidhaa muhimu katika kuongeza ajira kwa wananchi wa jimbo hilo.

Ridhwani alitoa msimamo wake huo juzi ikiwa ni sehemu ya mkakati wake wa kuinua maisha ya wakazi wa Chalinze kwa njia ya sanaa na michezo.

Akizungumzia fursa za ajira katika sanaa na michezo, alisema anaamini Chalinze kuna vipaji vingi ambavyo vinatakiwa kuendelezwa.

Alisema akiwa kama mgombea wa Ubunge analitambua hilo na anaona kuwa linahitaji kuandaliwa mkakati endelevu.

"Mimi mwenyewe kwanza ni mdau wa mambo mengi, yaani mimi kwanza ni mtu wa mpira na pia masuala ya utamaduni, ninaamini kabisa katika mila zetu za kiafrika, sasa kwa nini nisipiganie kukuza sekta hizi," alihoji.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...