https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, March 30, 2014

Pendo Njau:Tanzania sina mpinzani

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

BONDIA wa ngumi na mateke nchini (Kick Boxing), Pendo Njau, amesema kwamba kwa Tanzania imekuwa ngumu kupata mapambano ya kuonyesha uwezo wake, hali inayompa wakati mgumu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Pendo alisema kuwa wanawake wengi wameshindwa kupata mwamko wa kuingia katika mchezo huo unaozidi kushuka thamani yake siku hadi siku.

Alisema changamoto za ukosefu wa watu wa kupanda nao ulingoni kwenye ngumi na mateke ndio zilizomfanya Japhet Kaseba ahamie upande wa ngumi za kawaida kwa ajili ya kutafuta maslahi.

“Ili uwe bondia mzuri lazima uwe na watu wa kupanda nao ulingoni, hivyo kwa upande wetu wa ngumi na mateke, changamoto za kukosa wanawake wa kupigana nao kunaleta utata.

“Naumiza kichwa jinsi ya kulinda kiwango changu bila kupanda ulingoni, hivyo huu ni wakati wa kutafakari kwa kina mfumo wangu wa maisha,” alisema.

Pendo anatokea katika klabu ya ngumi ya Kaseba, ambaye leo anacheza na Thomas Mashali, katika Ukumbi wa PTA Sabasaba, jijini Dar es Salaam.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...