https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, March 26, 2014

Kaseba:Nimepata dawa ya Mashali



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BONDIA wa ngumi za kulipwa hapa nchini, Japhet Kaseba, amesema kwamba tayari ameshapata dawa nzuri ya kumtandika mpinzani wake Thomas Mashali, katika pambano linalotarajiwa kupigwa Machi 29, katika Ukumbi wa PTA Sabasaba, jijini Dar es Salaam.
Pambano hilo linalogusa hisia za wengi, linasubiriwa kwa hamu na wadau wengi, huku kila mmoja akiwa na imani ya bondia wake kuibuka na ushindi.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Kaseba alisema kwamba amepata dawa sahihi ya kumpiga mpinzani wake, baada ya kugundua udhaifu wake.
Alisema mara kadhaa Mashali amekuwa bondia ambaye ana uwezo mzuri, lakini huwa anaingiza uhuni anapokuwa ulingoni, jambo linalomfanya yeye awe makini zaidi.
“Nimepata dawa ya kumpiga Mashali ikiwa ni pamoja na kuzalisha matamanio zaidi ya kuibuka na ushindi katika pambano hilo.
“Naamini hatakuwa na madhara yoyote katika yangu, hivyo sina shaka maandalizi ninayofanya yataniweka kileleni, ukizingatia kuwa nina mipango kabambe katika tasnia ya masumbwi hapa nchini,” alisema.
Aidha, Mashali yeye alikaririwa na vyombo vya habari kuwa hana hofu juu ya pambano lake, akiamini kuwa atamziba mdomo Kaseba.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...