https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, March 23, 2014

Azam yashinda, Simba yalala mbele ya Coastal Union Wagosi wa kaya

TIMU ya Azam FC ya jijini Dar es Salaam, imejiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kuwania ubingwa wa Tanzania Bara, baada ya kuifunga JKT Oljoro bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodaco uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam.

Bao la Azam lilifungwa katika dakika ya 71 na mshambuliaji wa timu hiyo, John Bocco kali.
Kwa matokeo hayo wanaendelea kukalia usukani wa ligi hiyo wakiwa na pointi 47,  kwa tofauti ya pointi nne na Yanga, wenye pointi 43.

Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo uliochezwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, timu ya Simba ilijikuta ikifungwa bao 1-0 dhidi ya Coastal Union ya Tanga.

Bao la Coastal Union katika mchezo huo lilifungwa katika dakika ya 45 na Hamadi Juma baada ya kuwazidi ujanja mabeki wa Simba na kumchambua kipa Ivo Mapunda.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...