https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, March 23, 2014

TAZARA wafungua tawi la Simba SC, wapewa onyo la kutokuwa wachochezi ili waisaidie klabu yao



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
WAFANYAKAZI 176 wa Shirika la Reli la Zambia na Tanzania (TAZARA), wamejiunganisha kwa pamoja na kufungua tawi la klabu ya Simba, wakiwa na shauku ya kuisaidia timu yao kufanya vyema na wao kupata raha ya ushindi.
Baadhi ya wanachama wa Tawi la TAZARA wakisikiliza maneno ya meza ya mbele.
Uzinduzi wa tawi hilo ulikwenda sambamba na kugawa kadi 50 za uanachama kwa wafanyakazi hao, huku mgeni rasmi akiwa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya klabu hiyo, Swed Mkwabi.


Swed Mkwabi, mwenye fulana nyekundu, akipiga picha ya pamoja na wanachama wa tawi la Simba la TAZARA leo jijini Dar es Salaam
Akizungumza katika uzinduzi huo, Katibu wa Tawi hilo jipya la Simba lililokuwa na maskani yake TAZARA, Abdallah Sambizi, alisema kuwa kuanzishwa kwa tawi hilo ni hatua muhimu za kuisaidia klabu yao.



Mgeni Rasmi, aliyesimama meza ya mbele, Swed Mkwabi, akisikiliza baadhi ya hoja kutoka kwa wanachama wa Simba, Tawi la TAZARA, jijini Dar es Salaam leo.
Alisema kuwa wanaamini kwa pamoja watafanya mambo mema ya kusaidiana na viongozi wao Makao Makuu kwa ajili ya kuipaisha timu yao, ambayo kwa msimu huu imeonekana kusua sua.

Sisi mashabiki na wanachama tunachohitaji ni ushindi tu, hivyo naamini kwa pamoja tutashirikiana na wenzetu wa Makao Makuu ili kuipaisha klabu yetu ndani na nje ya nchi, huku tukiepuka kuwa wasumbufu au kutoa matamko yasiyokuwa na mashiko kwa timu yetu tunayoipenda,” alisema Sambizi.

Naye Mgeni rasmi wa uzinduzi wa tawi hilo, Mkwabi, aliwataka wanachama na viongozi wa tawi hilo kuwa na dhamira ya kweli ya kuisaidia Simba na sio wao kusaidiwa na klabu yao kwa kushiriki au kujitolea kwa mambo ya kimaendeleo.

TAZARA msisubiri mlipe ada tu ya Sh 1000 kwa mwezi badala yake muingie sasa kwa kushiriki mambo mazuri, hasa ya kununua bidhaa halali za Simba ambapo hayo ndio maendeleo makubwa,” alisema.

Viongozi wa tawi hilo ni pamoja na Mwenyekiti Hemed Msangi, Makamu Mwenyekiti Amri Hussein, Katibu Sambizi, Katibu Msaidizi ni Gabriel Samson, Katibu Mwenezi ni Alfred Mdemu, Mweka Hazina ni Kijakazi Herith, wajumbe ni Nicholaus Bukuku, Khatibu Makata, Heronima Maganga.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...