https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, March 30, 2014

DC Rweyemamu asisitiza umuhimu wa michezo wilayani Handeni


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

MKUU wa wilaya Handeni, Muhingo Rweyemamu, amesisitiza umuhimu wa jamii kuweka mkazo katika kuibua vipaji kwa ajili ya maendeleo ya vijana na wanaoshiriki katika sekta ya michezo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam hivi karibuni, DC Rweyemamu, pichani, alisema kuwa vipaji ni muhimu kuendelezwa kwa maendeleo ya Tanzania kwa ujumla.

Alisema hali hiyo inamfanya aweke mipango ya kuanzisha mashindano mbalimbali, hasa yanayoshirikisha vijana wadogo kwa kuwakuza kimichezo.

“Hii ni changamoto na dhamira ya kila mmoja wetu kufanya juhudi za kuendeleza vipaji vya vijana wetu kwa ajili ya kuwapatia mwanga mzuri.

“Hii ndio sababu tunajaribu kuwaza namna ya kuhakikisha watoto wote wanaanza kucheza tangu wakiwa katika shule za msingi,” alisema.

Kwa mujibu wa DC Rweyemamu, anajipanga kuanzisha mashindano ya vijana wadogo kwa ajili ya kuwakuza katika minajiri ya kuboresha vipaji vyao.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...