https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, April 25, 2013

Warembo wachangamkia ushiriki wa Miss Kibaha 2013



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
WAREMBO wamejitokeza katika kushiriki shindano lijalo la Redds Miss Kibaha 2013.
AKhadija Kalili, Mkurugenzi wa Linda Media Solution
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Kampuni ya Linda Media Solution (LIMSO), ambaye pia ndio Mratibu wa shindano hilo Khadija Kalili alisema amefurahishwa na mwitikio wa warembo waliojitokeza hadi sasa katika kuwania taji la Miss Kibaha.
 
“Mwitikio wa warembo kwa kweli unatia moyo hivyo kwa kuwa muda wa kufunga milango ya kupokea warembo bado iko wazi, mrembo yoyote anayejiamini kwamba ana vigezo anakaribishwa. Tunataka shindano la mwaka huu liwe na ushindani zaidi,” alisema Kalili.

Kalili aliwataja baadhi ya warembo waliojitokeza kuwa ni Nzeran Kitano, Martina Kapaya, Asma Said, Maud Bernad, Flora Mlowola na Nancy James.
 
Warembo wengine ni Esther Albert, Beatrice Bahaya, Jenipher Njabiri na  Rachel John.
 
Warembo wa Miss Kinaha 2013 tayari wameanza mazoezi wakiwa chini ya wakufunzi wawili ambao ni Sweet Ray na Bob Rich.
 
Shindano la kumsaka Miss Kibaha litafanyika katika ukumbi wa Kontena uliopo Kibaha Maili Moja Mkoani Pwani.
 
Kalili aliongeza kwa kusema kuwa shindano la mwaka huu litaandika historia mpya ya urembo mkoani humo kwakuwa Kampuni ya LIMSO imejipanga hivyo mashabiki wa mashindano ya urembo wa Wialaya ya Kibaha na Mkoa wa Pwani kwa ujumla wakae mkao wa kupata raha.
 
“Shindano la mwaka huu litakuwa la  aina yake kulinganisha na mashindano ya miaka ya nyuma kwani mwaka huu LIMSO imejipanga” alijigamba Kalili.
 
Kalili anawataja baadhi ya wadhamini waliojitokeza kudhamini shindano hilo ni Fredito Entertainment, CXC Africa,Michuzi Blog , The African Stars Entertainment (ASET) na Redds Premium Cold.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...