https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, April 25, 2013

January Makamba azuia watoa uchawi jimboni kwake Bumbuli



Na Mwandishi Wetu
MBUNGE wa Bumbuli kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), January Makamba, ameelezea kusikitishwa kwake na masuala ya imani ya kishirikina kupiga hodi kwenye Jimbo lake.

January Makamba, Mbunge wa Bumbuli
Akielezea kwa kina kwenye akaunti yake ya facebook, Makamba alisema kuwa Ijumaa na Jumamosi walikwenda Bumbuli watu wanaodai wana uwezo wa kutoa wachawi na kuamua kuwachangisha watu fedha kwa ajili ya zoezi hilo na kudhalilisha wazee na kina mama wengi na kusababisha  wanyanyaswe na kufanyiwa fujo.
January Makamba kushoto akizungumza na baadhi ya wananchi wake jimboni Bumbuli hivi karibuni.
Alisema kuwa baada ya kuona hivyo, aliamua kuzungumza na viongozi na Mkuu wa Wilaya kwamba watu hao wafukuzwe mara moja na wakamatwe kwasababu zoezi hilo ni kinyume cha Sheria za nchi.

"Vilevile, katika zama hizi mambo ya uchawi na kutafuta wachawi hayana nafasi kabisa. Ni mambo ambayo yametubakiza nyuma kimaendeleo miaka nenda rudi.
"Baada ya witch-hunters kufukuzwa kuna baadhi ya vijana walioratibu ujio wao walienda kituo cha polisi Bumbuli na kujaribu kung'oa dirisha na kuvunja mlango. Kituo cha Polisi hakijachomwa moto. Pia wakaenda kwenye Ofisi ya Afisa Tarafa na kujaribu kuvunja Ofisi," alisema Makamba.

Aliendelea kusema kuwa wote wamekatwa Jumapili na kupata message nyingi za wapiga kura wakimpongeza kwa kuzuia upuuzi na wengine wakitaka waruhusiwe watoa uchawi.

"Kama viongozi, tunayo kazi kubwa ya kuelimisha watu kuhusu hizi imani.
Changamoto kwetu kule sio tu masuala ya barabara, maji, umeme, nk lakini pia haya masuala. Bahati mbaya imani za kichawi zimeshamiri sana kwenye jamii nyingi za Kiafrika na kazi ya kuziondoa ni kubwa sana.

"Mara nyingi zinatokana na maendeleo kuwa duni lakini vilevile imani hizo ni chanzo cha maendeleo duni. Hadithi ya kuku na yai kipi kilianza, bahati nzuri hali imetulia. Kilifanyika kikao cha Madiwani wote, wenyeviti wote wa vijiji na Watendaji wa Kata na Maafisa Tarafa kuweka msimamo wa pamoja kuhusu haya masuala ikiwemo elimu kwa umma," alisema.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...