https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, February 16, 2014

Wilaya ya Handeni yaona haya kuomba omba chakula, yahimiza wananchi wajiwekee akiba



Na Mwandishi Wetu, Handeni
MKUU wa wilaya Handeni, Muhingo Rweyemamu, amesema kwamba ni aibu kubwa kwa wilaya yake kuomba chakula lich licha ya kuzalisha chakula kingi kwa mwaka.
Akizungumza na Handeni Kwetu Blog wilayani hapa, Rweyemamu alisema kuwa hali hiyo inampa wakati mgumu, maana wao ni miongoni mwa wilaya zinazoheshimika katika kuzalisha zao la mahindi.

Alisema wafanyabiashara wengi wanaingia Handeni kununua mahindi, hivyo ni wakati wao sasa kuliangalia jambo hilo kwa kina na kuleta tija.

“Kwanza lazima tupige vita kuuza mahindi bila kuweka akiba yetu na familia zetu, maana huo ni mpango mbaya unaotufanya tuombe chakula kila mwaka.

“Nikienda mjini kuomba omba chakula napata wakati kwasababu tuna ardhi ya kutosha na wakulima wetu wengi wanalima, ila mwisho wa siku wanauza hadi akiba za kula wao na watoto wao,” alisema Rweyemamu.

Kwa mujibu wa Rweyemamu, wananchi wote na wakazi wa Handeni wanapaswa walime sana, huku wakijiwekea akiba badala ya kuuza chakula chao, hivyo kuifanya wilaya hiyo ikumbwe na njaa kila wakati.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...