https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, February 23, 2014

Simba majanga, yapigwa 3-2 na Ruvu JKT, Azam nao watoka sare dhidi ya Prisons



MAJANGA. Timu ya Simba ilijikuta ikiangukia pua baada ya kukubali kipigo cha bao 3-2 kutoka kwa maafande wa JKT Ruvu, mechi iliyopigwa katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, hivyo kuonekana kujitoa rasmi kwenye mbio za ubingwa.
 Wachezaji wa JKT Ruvu wakishangilia goli dhidi ya Simba.
Mabao ya JKT yalifungwa na Hussein Bunu dakika ya 13, Dakika ya 45 kupitia kwa Emmanuel Swita na dakika 52 kupitia kwa Swita tena, wakati mabao ya Simba yalifungwa na Amis Tambwe dakika ya 64 na 84, hivyo kulala bao 3-2.

Mechi nyingine iliyopigwa leo ni Azam FC na Tanzania Prisons ambazo zote zimefungana bao 2-2 katika mechi iliyokuwa na msisimko wa aina yake.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...