https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, February 23, 2014

Moto wazuka baada ya magari mawili kugongana uso kwa uso mkoani Morogoro

LEO asubuhi mkoani Morogoro kumetokea ajali iliyohusisha Lori lililokuwa limebeba mafuta ya diesel, ambalo limegongana na lori lililokuwa likifuata saruji tanga na kusababisha shoti iliyozusha moto mkubwa eneo la Lubungo, Mikese. Ajali hiyo ilisababisha magari mengine yashindwe kupita kwa zaidi ya saa tatu.
Moto ukitekeza magari yaliyogongana mkoani Morogoro leo.
Shuhuda wa ajali hiyo alisema kuna uwezekano mkubwa ajali hiyo ikagharimu uhai wa mtu, hasa kwa kuangalia mazingira yake, hasa kwa madereva. Taarifa kamili juu ya ajali hiyo tutaendelea kukupatia kadri zitakavyofika kwenye chumba chetu cha habari.

Mtu mmoja akiangalia moto ulivyokuwa unatekeza magari yaliyogongana uso kwa uso leo mkoani Morogoro....

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...