https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, February 15, 2014

Mbeya City waidindia Simba, kama ilivyofanya kwa Yanga kwa kutoka sare ya bao 1-1 mjini Mbeya



TIMU ya Mbeya City imeshindwa kuutumia uwanja wake wa nyumbani wa Sokoine, mjini Mbeya, baada ya kulazimishwa sare na Simba SC, katika mechi iliyomalizika kwa kufungana bao 1-1.

Bao la Mbeya City lilifungwa na Deogratius  Julius dakika ya 14, wakati Simba walisawazisha kwa kupitia Amis Tambwe, dakika ya 50. Kwa ujumla mchezo ulikuwa na ushindani, ambapo pia kunyesha kwa mvua ndani ya uwanja huo ulisababisha wachezaji kuteleza uwanjani.

Mbeya City watabidi wajilaumu sana kwa kushindwa kutoka na ushindi mbele ya Simba, ukizingatia kuwa wao walikuwa na sababu zote za kushinda kutokana na maandalizi yao sambamba na ari ya vijana wao.

Matokeo hayo hayana tofauti na siku walipocheza na Yanga, ambapo zilitoka sare ya bao 1-1 katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, katika mfululizo wa Ligi ya Tanzania Bara.
 

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...