https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, February 07, 2014

Wacomoro wawaogopa Okwi, Ngassa

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

WINGA wa timu ya Yanga, Mrisho Ngassa na mshambuliaji wake Emmanuel Okwi, ndiyo wachezaji wanaoogopwa na wachezaji wa timu ya Komorozine ya nchini Comoro, watakapokutana kesho Jumamosi, katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Dalaam, ikiwa ni mbio za Ligi ya Mabingwa Afrika.


Mechi hiyo ya kwanza katika michuano hiyo, inaanza huku Yanga wakitumainiwa kuvuka raundi ya pili kutokana na uwezo wa wachezaji wake dhidi ya vijana hao wa Comoro.


Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Nahodha wa timu ya Komorozine, Er Feda Rohaned, alisema kuwa wamekuwa na shauku sana ya kumdhibiti Ngassa na Okwi ili wasilete madhara katika mechi yao ya raundi ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.


Alisema kuwa wanafahamu ubora halisi wa Ngassa na namna ya kukabiliana naye ndani ya uwanja katika mchezo wao muhimu wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa.


“Tunamuhofia Ngassa na Okwi kwasababu ni wachezaji wazuri na wenye uwezo wa kufanya makubwa uwanjani, lakini sisi tumejipanga kukumbana nao.


“Tunaamini wachezaji wote wa Komorozine tutafanya kazi kwa bidii kuwania ushindi dhidi ya Yanga, ambayo inaanza katika uwanja wa nyumbani kwao dhidi yetu,” alisema.


Wacomoro hao wanaanza kwa mkosi wa kukumbana na Yanga yenye kila dalili ya uchu wa ushindi katika mechi hiyo muhimu ili ifuzu hatua ya pili ya michuano hiyo ya Kimataifa.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...