https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, November 03, 2013

Malinzi:Simba na Yanga kukiona cha moto


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

 RAIS wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Jamal Malinzi, amevitaka vilabu vya soka vya Simba na Yanga kukubali matokeo ya uwanjani ili wasiingie kwenye mgogoro kwakuwa ofisi yake watakuwa wakali dhidi yao.

Rais wa TFF, Jamal Malinzi, pichani.
Malinzi aliyasema hayo katika makabidhiano ya ofisi kutoka kwa rais aliyemaliza muda wake, Leodgar Tenga, huku yakihudhuriwa na watu mbalimbali kwa ajili ya kushuhudia tukio hilo la aina yake.


Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Malinzi alisema watakaokiuka sheria zitawabana, huku akitumia muda mwingi kuwataka Simba na Yanga wakubali matokeo na kuacha kufanya vurugu.


Alisema yoyote atakayefanya mambo kinyume sheria hazitawaacha watambe, hivyo mchezo wowote utakapokuwa unafanyika mwamuzi ndiyo anakuwa mtu wa mwisho kwenye patashika hiyo.

“Sisi wote ni mashuhuda katika tukio la kufanya vurugu ndani ya uwanja, mechi ya Simba na Kagera Sugar, hivyo lazima tujuwe kuwa hata sekunde za  mwisho za mchezo wowote, bado mwamuzi ndio mtu wa mwisho.


“Naomba niseme kuwa tutakuwa wakali katika suala lolote litakalofanywa kinyume, hivyo nadhani dawa ni kwa timu kujiandaa vizuri badala ya kusubiri lawama kwa waamuzi na kufikia kuvunja viti,” alisema Malinzi.


Watu mbalimbali walihudhuria katika hafla ya makabidhiano hayo, akiwamo Mwenyekiti wa Baraza la Michezo BMT Dioninz Malinzi, Meya wa Manispaa ya Ilala, Jery Silaa na wengineo.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...