https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, November 02, 2013

Cheka:Umaarufu wangu unanipa uchungu



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BONDIA wa ngumi za kulipwa hapa nchini, Francis Cheka, amesema kwamba umaarufu wake unampa uchungu kwasababu hauendani na maisha halisi anayoishi kutokana na mchezo huo kutawaliwa na njaa ya kutisha.
Bondia Francis Cheka, pichani.
Akizungumza jana kwa njia ya simu akitokea mkoani Morogoro, Cheka alisema mfumo mzima wa maisha yake umekuwa wa njaa na hakuna kampuni inayofikiria namna ya kuingia naye mkataba ili afike mbali zaidi.

Alisema amekuwa akipata fedha kiduchu mara chache anapokuwa na pambano, huku gharama za maandalizi za mchezo huo kuwa kubwa na kumpa wasiwasi wa maisha yake ya baadaye atakapoachana na masumbwi.

Cheka alisema ukata huo ndio unaomfanya ashindwe kutembelea kaatika mikoa mbalimbali ya Tanzania kujionea hali ya masumbwi ilivyo sanjari na kushirikiana na wadau wengine kuweka mipango ya kimaendeleo.

“Hakika hali hii inanipa wasiwasi mkubwa, maana wakati mwingine maisha yanakuwa magumu na inashangaza kwanini nakuwa maarufu wakati ukata umeshika hatamu, hivyo suala hili linanipa wakati mgumu.

“Naomba wadau wa masumbwi na kampuni kuingia sasa kunisaidia, ukizingatia kuwa naandikwa na kutajwa mno, ilaa vipi thamani ya umaarufu wangu inaendana na maisha halisi ninayoishi ndani na nje ya masumbwi,” alisema.

Cheka ni miongoni mwa mabondia mahiri wanaotamba kwa kiasi kikubwa katika mchezo wa masumbwi, huku kila anayeingia naye ulingoni akifanikiwa kuibuka kidedea na kuitangaza nchi katika kona za Kimataifa.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...