https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, November 10, 2013

Malaika wamwagia sifa Mashauzi, Dully Sykes na Cassim Mganga


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

UONGOZI wa bendi ya Malaika, umejigamba kwa uwezo wa kundi la taarabu la Mashauzi Classic, sambamba na Cassim Mganga na Dully Sykes, wataosindikiza uzinduzi wao Novemba 15 katika Ukumbi wa Mzalendo Pub, Kijitonyama, jijini Dar es Salaam.


Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa bendi hiyo, Michael Rocky, alisema tayari wamekubaliana nao juu ya kushiriki katika uzinduzi wa bendi yao.


"Tuliwaomba kama wasanii wenzetu, walikubali na kutuahidi kutoa burudani nzuri katika onesho hilo maalumu la kuzaliwa kwa bendi mpya," alisema.

“Tuna nyimbo sita zilizofaniwa mazoezi, mbili zimerekodiwa, nne bado hazijarekodiwa, zote zitasikika siku ya uzinduzi wa bendi yetu," alisema Mkurugenzi huyo.


Bendi hiyo ya Malaika inaongozwa na Mfalme Christian Bella, Katibu Mkuu ni Andrew Sekedia akisaidiwa na Emmanuel Karonji 'Totoo Zebingwa’.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...