https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, November 04, 2013

CCM Kinondoni kunoana makali mjini Dodoma kwa siku nne

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) wilaya Kinondoni, kimeanza mikakati ya kuwanoa viongozi wake ili kuwapatia uzoefu wa kukitumikia chama kwa kipindi kijacho na hatimae kuwa na nguvu, kwa kuandaliwa semina itakayofanyika kesho (leo), mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa CCM wilaya Kinondoni, Salum Madenge, akiwa kwenye moja ya matukio ya kichama.
 Semina hiyo inahusu wenyeviti wa CCM wa Kata zilizopo wilayani Kinondoni, huku ikiwa na dhamira yaa kuhakikisha viongozi hao wanapewa uwezo wa kutimiza majukumu yao ya kila siku.

Akizungumza leo asubuhi wakati viongozi hao wanaelekea katika semina hiyo ya siku nne mjini Dodoma, Mwenyekiti wa CCM Wilaya Kinondoni, Salum Madenge, alisema kwamba siku zote malengo ya chama ni kushika dola, hivyo anaamini kwa kuandaliwa semina hiyo ni sehemu ya kujenga mfumo mzuri wa kiutendaji ndani ya chama chao.

Alisema ukiacha semina ya wenyeviti wa Kata Kinondoni, pia Makatibu wameshafanyiwa mpango huo, jambo ambalo linaonyesha mwendo mzuri wa chama chao.
“Chama chetu kina mwingiliano mzuri wa kiungozi na changamoto mbalimbali, hivyo utaratibu wa semina kwa viongozi wake ni mzuri kwakuwa unawapa nafasi ya kujitathimini mahali walipo na wanapoelekea.

“Tunaahidi kuwatumikia Watanzania wakati wowote kwa kuhakikisha kuwa kuanzia ngazi ya chini ya viongozi wetu hadi Taifa wanafahamu wajibu wao na malengo ya kuwasimamia wananchi,” alisema Denga.

Semina hiyo imeandaliwa na CCM Kinondoni kwa kushirikiana kwa karibu na Mchumi wa Chama Cha Mapinduzi CCM Kata ya Makumbusho, Yusuph Mhandeni kwa ajili ya kuwapa mbinu mbalimbali wenyeviti hao ili waje kukitumikia chama kwa juhudi na maarifa.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...