https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, November 10, 2013

Benchi la ufundi lamuita Kaseja Yanga, asaini miaka miwili



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

UONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema kwamba benchi la ufundi chini ya Kocha wao Ernest Brandit, alipendekeza Juma Kaseja kusajiliwa ndani ya kikosi chao, jambo lililofanikiwa baada ya kuingia naye mkataba wa miaka miwili.

Msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto, pichani.
Usajili wa dirisha dogo wa Kaseja kwa timu ya Yanga, umepokelewa kwa hisia kali na mashabiki wa soka wa Tanzania, huku uongozi ukionekana kupongeza kwa nyota huyo kujiunga na timu yao kwa ajili ya mzunguuko wa pili.


Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto, alisema kwamba ni kweli wameingia naye mkataba wa miaka miwili kwa ajili ya kuitumikia klabu yao.


Alisema hatua ya kumsajili nyota huyo imetokana na mahitaji ya kocha wao aliyetaka kumnyakua kipa huyo mwenye uwezo mahiri wa kusimama langoni kwa umakini.


“Viongozi wa Yanga wanafanya usajili kwa kupewa nafasi na benchi la ufundi, hivyo walipomuhitaji Kaseja ndio taratibu zikafuatwa.


“Kaseja ni kipa mzuri hivyo tunaomba wanachama na mashabiki wa Yanga kumpokea kwa mikono miwili kwa ajili yaa kuitumikia timu yetu katika michuano ya mzunguuko wa pili na Ligi ya Mabingwa Afrika, baadaye mwakani,” alisema.


Awali alipoulizwa juu ya suala la kusajiliwa Kaseja, Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako alionyesha kupingana na madai hayo, akisema si kauli za viongozi.


“Acheni kusikiliza maneno kutoka vichochoroni huko, badala yake msikie kauli za viongozi, maana mengi yataendelea kusikika zaidi ya hayo ya Kaseja kusajiliwa na Yanga,” alisema.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...