https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, November 25, 2013

Malaika bendi yafanya kufuru bila Bellah mjini Tanga



Christian Bellah, Rais wa Malaika Bendi
Na Oscar Assenga, Tanga.

BENDI Mpya ya Mziki wa Dansi nchini Malaika Music Band jana iliweza kuwakonga nyoyo vilivyo mashabiki wake bila ya kuwepo kwa mwimbaji wao nguli Christian Bella katika onyesho ambalo lilifanyika kwenye ukumbi wa Tanga Hotel Jijini Tanga.

Onyesho hilo ambalo lilianza saa nne usiku lilikuwa la aina yake mara baada ya waimbaji wa bendi hiyo akiwemo Toto the Bingwa na wengine ambao kila mmoja aliweza kucheza kwa staili ya aina yake kitendo ambacho kilifanya mashabiki waliojitokeza kushuhudia onyesho hilo kulibuka kwa shangwe na nderemo.
Wakizungumzia onyesho hilo baadhi ya wakazi waliohudhuria walisema bendi hiyo ni moto wa kuotea mbalimbali licha ya kuwa mpya ambapo pia waliitabiria mafanikio makubwa kwa siku za usoni kutokana na kukamilika kila idara.

Edgar Mdime ambaye ni mkazi wa Chuda jijini Tanga alisema ladha nzuri waliokuwa wameikosa kwa muda mrefu waliweza kuipata siku hiyo kutokana na umahiri wa bendi hiyo kuanzia wapigaji vinanda,waimbaji na wachezaji hali iliyomlazimu kuhsindwa kukaa kwenye kiti na badala yake muda wote kucheza.
Mdime alisema kuanishwa kwa bendi hiyo kutaleta changamoto kubwa sana hapa nchini hasa kwa baadhi ya bendi ambazo zinafanya kazi kwa mazoezi na kuitaka kuendelea na kuwapa raha watanzania.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...