https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, November 18, 2013

Beatrice Mroki apata kipaimara kanisa la KKKT Ukonga

Novemba 17, 2013 ilikuwa siku ya furaha sana kwa Beatrice Mroki (kushoto) kwa kupata sakrementi yake ya Kipaimara baada ya kuhitimu mafunzo ya miaka miwili katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Ukonga jijini Dar es Salaam. Pichani ni Beatrice akigonganisha glasi na msimamizi wake Neema Steven wakati wa tafrija maalum ya kumpongeza iliyofanyika katika ukumbi wa Samunge Ukonga Mazizini.
 Hapa ilikuwa Kanisani wakisubiri kupokea Kipaimara katika KKKT Ukonga
Baada ya Kipaimara baba na mama yake Beatrice wakilamba picha na Binti yao.
 Nasisi tulijipiongeza kwa malezi bora Mungu aliyotujalia.
Bibi zake Beatrice wakijipongeza na kumtakia heri Mjukuu wao.
 Beatrice na wapambe wake...
Pongezi kutoka kwa wazazi...
 Dada Kilave akimpongeza mdogo wake
 Kikundi cha Ligimilo wakicheza kwaito...
Keki ilikuwa hiviii ...
 na ilikatwa hivi....
 Ikaliwa hivi... Hapa Beatrice akimlisha mdogo wake Glory.
 Father Kidevu wakati wa zawadi alimpa gwala binti yake
Muongezaji maarufu wa filamu za Kibongo Leah Mwendamseke nae alikuwepo.
 Ligimilo wakitangaza zawadi yao..
Weee...!! Tulia nami nimsaidie baba leo...Glory Mroki akimfotoa dadayake picha.
 Kazawadi haka jamani... siku moja nitavaa shati lake.
 Huko jikoni mambo yalikuwa hivi
 Mwisho lilishuka sebene kali kutoka kila aina ya muziki kuanzia injili hadi katika kiduku namna hii.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...