https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, October 07, 2013

Gurumo: Sijakimbia zogo Msondo Ngoma

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MWANAMUZIKI mkongwe hapa nchini, Muhidin Gurumo, amesema kwamba wapo wanaofikiri kuwa ameachana na muziki kwa ajili ya kukwepa migogoro katika bendi yake ya Msondo Ngoma, jambo ambalo si kweli.
Muhidin Gurumo, pichani.
Badala yake aliamua kuachana na muziki kwa kutangaza kustaafu kwasababu ya umri wake kuwa mkubwa sambamba na afya yake kuwa si nzuri, hivyo kujiweka kando katika muziki wa dansi.

Akizungumza mwishoni mwa wiki iliyopita, Gurumo alisema kuwa mara kadhaa muziki wa dansi unahitaji muda na pumzi za kutosha, hivyo kwake ilikuwa ni ngumu kufanya hivyo wakati wote.

Alisema muda wote Msondo Ngoma wamekuwa wakiishi kwa upendo kwa wanamuziki wote, hivyo kustaafu kwake ni njia ya kumfanya afikirie namna ya kuishi nje ya muziki.

“Kuna wakati bendi inakuwa 'busy' kupita kiasi kama vile kuandaa albamu, kufanya shoo na safari za kila aina, hivyo kwangu mimi nisingeweza tena kufanya hayo kutokana na afya yangu.

“Naomba wadau wote wajuwe namna gani nimeamua kukaa kando kwa ridhaa yangu na sio kukimbia mgogoro ambao si kweli, ukizingatia kuwa nimefanya kazi Msondo kwa miaka mingi mno,” alisema.

Kwa sasa kumeandaliwa shoo maalumu ya kumuaga mwanamuziki huyo, ikiwa chini ya mwenyekiti wa Kamati hiyo Asha Baraka, sanjari na wadau kadhaa wa muziki wa dansi nchini.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...