https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, October 27, 2013

Baba yake Wema Sepetu afariki Dunia leo Hospitali ya TMJ

Balozi Abraham Isaac Sepetu amefariki Dunia mapema leo akiwa katika Hospitali ya TMJ alikokuwa amelazwa akitibiwa ugonjwa wa Kisukari na kiharusi alioupata hivi karibuni mjini Zanzibar. 

Balozi Sepetu, ambaye pia ni baba mzazi wa Miss Tanzania 2006, Wema Isaac Sepetu, hadi anapatwa na ugonjwa na hatimaye mauti, alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Uwekezaji wa Vitega Uchumi Zanzibar.

Taarifa zaidi za msiba huo zitaendelea kukujia kadri zitakavyofika katika meza yetu, huku tukiamini kuwa msiba huo utakuwa umegusa hisia za wengi, wakiwamo mashabiki wa sanaa wa mwanadada Wema Sepetu.

 

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...