https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, October 24, 2013

Mgambo auawa na askari polisi apigwa risasi katika vurugu wilayani Kilindi mkoani Tanga

KIJIJI cha Lulago, wilayani Kilindi mkoani Tanga, kimeingia katika hofu kubwa baada ya mgambo Mbwana Salim kuuawa kutokana na kutoelewana katika moja ya majukumu yake kikazi, huku askari polisi naye akipigwa risasi ya tumbo.
Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Costantine Masawe, pichani. Picha na Maktaba Yetu.
Baada ya kuuliwa kwa mgambo huyo na watu wasiofahamika, askari polisi waliingia na mmoja wapo kujikuta akipigwa risasi ya tumbo katika kadhia hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa za awali katika kijiji hicho, sakata hilo lilianzia kwenye vurugu za wafanyabiashara ambao inasemekana waligoma kulipa ushuru.

Kamanda wa Polisi Mkoa Tanga, Costantine Masawe, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo wilayani Kilindi mkoani Tanga.

“Taarifa hizo zimetufikia kutokana na askari wetu kupigwa risasi wakati anajaribu kutimiza majukumu yake na taarifa zaidi tutaendelea kuzitoa juu ya tukio hilo,” alisema.

Kamanda Masawe alisema baada ya kutokea vurugu hizo na mgambo kuuliwa, askari waliingia na kufukuzana na watu wanaosadikiwa kuwa walishiriki kwenye tukio hilo, ambapo mwisho wake ulifikia kwa askari kupigwa risasi ya tumbo na sasa yupo hospitali akipatiwa matibabu.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...