https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, October 28, 2013

Coastal Union yainyunyizia vitatu Mtibwa Sugar jijini Tanga leo

Na Oscar Assenga,Tanga.

TIMU ya Coastal Union ya Tanga leo wakiwa chini ya Kocha Joseph Lazaro wamefanikiwa kuibamiza Mtibwa Sugar mabao 3-0,katika mchezo wa ligi kuu Tanzania bara uliochezwa uwanja w a Mkwakwani mjini hapa.

Kikosi cha Coastal Union kilichoichapa Mtibwa Sugar mabao 3-0.
Wachezaji wakisalimiana kabla ya mchezo huo kuanza.
Wachezaji wakiingia uwanjani.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa mkali na wenye upinzani mkubwa ambapo Coastal Union waliweza kuandika bao lao la kwanza kwenye dakika ya 20 kupitia Crispian Odulla aliyemalizia kazi nzuri iliyofanywa na Haruna Moshi “Boban’



Baada ya kuingia bao hilo,Coastal Union waliweza kuendeleza wimbi la mashambulizi langoni mwa Mtibwa Sugar na kufanikiwa kuongeza bao la pili lililofungwa dakika ya 38 kupitia Jerry Santo kwa njia ya penati iliyotokana na Keneth Masumbuko wa Coastal Union kuangushwa katika eneo la hatari na Yusuph Nguya wa Mtibwa Sugar na mwamuzi wa mchezo huo Hashim Abdallah kuamuru ipigwe penati.



Mpaka timu zote zinakwenda mapumziko Coastal Union walikuwa wakiongoza kwa bao 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar ambapo kipindi cha pili kilianza kwa kasi kwa kila timu kuingia uwanjani hapo zikiwa na hari mpya baada ya kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake.



Wakionekana kujipanga baada ya kufanya mabadiliko kwa kuwatoa baadhi ya wachezaji wake wakiwemo Dickson Mbeikya na kumuingiza Jamal Mnyate hali ambaye iliweza kukiongezea nguvu kikosi hicho.



Kutokana na mabadiliko hayo,Mtibwa Sugar waliweza kujipanga na kupeleka mashambulizi langoni mwa Coastal Union lakini Mlinda mlango wake,Shabani Kado aliweza kuwa shujaa kwa kupangua mashuti makali ambayo yalikuwa yakiekezwa langoni lake.



Kwa kuonyesha wao wanacheza kwa umakini mkubwa,Coastal Union waliweza kubadilisha aina ya mchezo ambao walikuwa wakioncheza hapo awali na kufanikiwa kulishambulia lango la Mtibwa Sugar kwa dakika kadhaa na hatimaye Coastal Union kuweza kuhitimisha karamu ya mabao langoni mwa Mtibwa kupitia Daniel Lyanga baada ya kutokea piga ni kupige langoni mwa timu hiyo.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...