https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, October 09, 2013

Chama cha CUF wilayani Mkinga chaweka mkakati mzito

Na Oscar Assenga, Mkinga
CHAMA cha Wananchi CUF wilayani Mkinga kimeelezea mikakati yake ya kufanya mikutano ya hadhara katika kata zote zilizopo wilayani humo lengo likiwa kukiimarisha chama hicho pamoja na kujiandaa na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ili kuchukua kata zote.

Akizungumza hivi karibuni,Mwenyekiti wa Chama hicho,Mauya Kileo amesema anaamini lengo lao litafanikiwa kutokana na kukabalika vilivyo na wananchi maeneo mbalimbali wilayani humo kitendo ambacho kiliwawezesha chama hicho kupata kata saba kati ya 21 zilizopo.

Kileo amezitaja kata ambazo zimechukuliwa na chama hicho wilayani humo kuwa ni Mtimbwani, Kwale, Manza, Boma, Doda, Moa na Duga Sigaya na kueleza mikakati yao ni kuongeza idadi ya kata kwenye uchaguzi huo mkuu kwani hilo linawezekana kutokana na mshikamano walionao.

Aidha aliwataka wanachama wa chama hicho kuendelea kuonyesha mshikamano ili kuweza kufanikisha malengo yao ya siku moja kuongoza halmashauri yaweze kufanikiwa.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...