https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, October 31, 2013

January Makamba azipiga tafu shule za sekondari Baga na Tamota


Na Raisa Saidi, Bumbuli,  

Mbunge  wa  jimbo  la  Bumbuli  January Makamba  amekabidhi  msaada  wa  shilingi  milioni mbili  katika  shule  ya  sekondari  ya Baga na  Tamota   kwa  ajili  ya  ujenzi  wa  Maabara   kwa lengo la  kuinua  masomo  ya  sayansi.



Pamoja na msaada huo wa milioni moja moja kwa kila shule pia ametoa  msaada  wa  mabati  mia moja kwa kila shule kwa ajili ya  kuezekea  vyumba  vya  madarasa  na nyumba  za walimu   katika  shule hizo.



Alitoa msaada huo wakati alipokuwa mgeni rasmi kwenye mahafali ya kidato cha nne kwenye shule hizo.

Makamba  ambae  pia  ni  Naibu  Waziri wa  Mawasiliano  Sayansi  na  Tenknolojia  alisema  kuwa  lengo  la  kutoa  misaada  hiyo  ni  kutaka  kuongeza  na  kuinua  kiwango  cha   elimu   katika  shule   zilizopo  katika  jimbo hilo.



Mbunge huyo  alisema kuwa msaasa huo ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa serikali katika kuhakikisha kila shule ya kata inakuwa na  maabara katika kuhakikisha kiwango cha ufaulu na hususani katika masomo ya sayansi hapa nchini kinaongezeka.



Wazazi na walimu wa Shule hizo  wameeleza kufurahishwa kwao na juhudi za Mbunge wa Jimbo hilo, January Makamba katika kukukuza kiwango cha elimu na kuondokana na usemi usemao Wasambaa hawajasoma na ni watu wa sokoni tu.


 Diwani wa kata ya Milingano Hozza Mandia akiwa katika mahafali hayo alisema kuwa juhudi  za Mbunge huyo ni  mfano mzuri  wa  kuigwa  na  wanasiasa  wengine  ili  kuwaletea  maendeleo   wananchi huku akiongeza kuwa  jitihada  hizo zinapaswa kuungwa mkono.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...