https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, October 26, 2013

Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa akoleza moto wa urais TFF

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

WAZIRI Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, amewataka wajumbe wa Mkutano wa Mkuu wa Shgirikisho la Soka nchini (TFF), kufanya uamuzi sahihi kwa kuchagua viongozi makini katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Jumapili, katika Ukumbi wa Golden Tower, jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, pichani.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa katika vyombo vya habari na Lowassa, wajumbe kufanya uamuzi mzuri katika uchaguzi huo ni hatua ya kukuza soka la Tanzania.


Alisema kuwa hatua hiyo inatokana na rais wa sasa, Leodgar Tenga kumaliza muda wake na kuanza mchakato wa kupatikana mrithi wake katika uchaguzi ulioandaliwa na Shirikisho hilo, huku nafasi ya urais ikiwaniwa na Athuman Nyamlani na Jamal Malinzi.


“Nikiwa Kama mmoja wa wadau wa mchezo wa soka, nimekuwa nikifuatilia harakati za kuelekea Uchaguzi Mkuu wa TFF siku ya jumapili, ambapo ni
siku muhimu kwa soka la Tanzania.


“Ni siku ambayo wajumbe watatuchagulia viongozi wa kuliongoza soka letu na kuendeleza juhudi za Rais wetu Dk. Jakaya Kikwete katika kusaidia mpira wa miguu hapa nchini,” ilisema taarifa hiyo.


Lowassaa
liwaomba wajumbe wachaguwe watu watakao endeleza juhudi hizo zenye kuhakikisha kuwa mpira wa miguu unasonga mbele na kulitangaza Taifa katika Nyanja za Kimataifa.


Aidha, Lowassa pia alimpongeza Tenga kwa kuweka msingi imara kuliongoza soka la Tanzania, akiamini ndio mchezo unaopendwa na watu wengi, hivyo kutaka sheria zifuatwe, huku tukilazimika kuingia kwenye mfumo wa utendaji unaolazimisha kupatikana kwa maalum za soka.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...